Na. Oliver Mathias
![]() |
| Muigizaji na mchekeshaji wa Hollywood, Kevin Hart akiwa na mkewe Eniko. |
Muigizaji na mchekeshaji wa Hollywood, Kevin Hart ambaye alikumbwa na shetani la kumsaliti mke wake ametumia show aliyofanya huko Georgia siku ya Jumapili iliyopita kwa kuiomba radhi familia yake.
Katika show hiyo Hart mwenye umri wa miaka 38, alianza kwa kusema “We got a lot of s*** to talk about, people,” kisha akamaliza kwa kuahidi kuwa mwaminifu ‘I’m going to be a better man,’.
Ndoa ya Hart na Eniko ina mwaka mmoja na tayari imeshakuwa na janga la usaliti na mwanamke aitwaye Montia Sabbag. Kabla ya kumuoa Eniko, Kevin amewahi kumsaliti mke wake wa kwanza.

No comments:
Post a Comment