Na.Erick
Kelvin
Mchekeshaji maarufu nchini Tanzania Emmanuel Mathias
maarufu kama MC Pilipili anepata ajali ya gari alipokuwa akitoka Mwanza
kuelekea Shinyanga.
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Saimoni Haule amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo katika kijiji cha Mwanishoni kata ya Bumiki wilayani Kishapu na amesema ajali hiyo ilitokea majira ya saa kumi alasiri na kuhusisha gari binafsi yenye namba za usajili T 362 BAE Toyota Prado, iliyokuwa na watu watatu dereva aliyejulikana kwa jina la Said Hasani mkazi wa Dar es salaam, kamanda Haule amesema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva na majeruhi wanaendelea kupatiwa matibabu hospitali ya Bugando.
Afisa mahusiano wa hspitali ya Bugando Luki Joseph amethibitisha kupokea majeruhi watatu na miongoni mwa majeruhi hao ni MC Pilipili, amesema kwa sasa wanaendelea vizuri na hali zao zinaewndelea kuimarika.
No comments:
Post a Comment