Na.
Joseph Abel
Licha ya juhudi nyingi zinazofanywa na serikaali kwa
kushirikiana na taasisi binafsi juu ya kudhbiti vitendo vya ukeketaji lakini bado ni
changaamoto kubwa katika jamii nyingi nchini Tanzania.
Mratibu wa masomo katika chuo cha uandishi wa habari cha TIME School of Journalism (TSJ), Blandina Semaganga amesema kuwa, vitendo hivi ni hatari kwa afya ya binadamu sababu vinaweza kupelekea kifo cha mama hasa pale anapojifungua.
“ hili suala bado makabila mengi wana lipractise na halitakiwi kiafya, sababu limekuwa likileta madhara kwa wanawake hasa wakati wa kujifungua,mama anapofikia wakati wa kujifungua hupoteza damu nyingi na hatimae mtoto anaweza kutoka salama lakini mama akapoteza maisha”.
Ameendelea kwa kusema, anaishukuru serikali kwa kufanikiwa
kupunguza vitendo hivi vya ukeketaji “ lakini kwa asilimia kubwa tunaishukuru
serikali kwa kupiga vita suala hili, tunaona linapotea taratibu ila sisemi
kama limeisha lakini bado kuna makabila wanafanya vitendo hivi” amesema
Semaganga.
Na kwa upande wake mwanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari cha (TSJ) Rodney Malongo amesema kuwa vitendo hivi vinapelekea kuenea kwa maambukizi ya magonjwa sababu kifaa kinachotumika ni kimoja.
“sababu nyingine ni kuenea kwa magonjwa kwa sababu chombo kinachotumika kufanya huo ukatili ni hikohiko kimoja kinazunguka kwa wanawake wengi” amesema mwanafunzi huyo
Aidha amesema Semaganga “ watanzania wote tunatakiwa kujali afya ya kila mmoja hasa afya ya mama, kwani mama ndio mlezi wa familia” amesema.
No comments:
Post a Comment